Mwili wa mwandishi wa habari za michezo wa gazeti la uhuru na mzalendo
Amina Athuman ukisafirishwa asubuhi hii na boti ya kilimanjaro kuelekea
Dar es Salaam na kusafirishwa hadi kijijini kwao Lushoto kwa mazishi
yanayotarajiwa kufanyika siku ya jumanne mchana. Marehemu alikuwa
Zanzibar kikazi akiripoti habari za michezo kombe la Mapinduzi na
kumkuta mauti hayo baada ya kujifungua mtoto wa kiume, kwa bahati mbaya
mtoto akafariki baada ya kuzaliwa na yeye kupata kifafa cha uzazi na
kufariki jana asubuhi. Mwenyenzi mungu ampe kauli thabiti na amsamehe
madhambi yake-Ameen
Sign up here with your email