MKOA WA MBEYA WAFIKIWA NA KOMPYUTA ZA BAYPORT - Rhevan Media

MKOA WA MBEYA WAFIKIWA NA KOMPYUTA ZA BAYPORT

Mratibu wa Masoko na Mawasiliano wa Bayport Financial Services, Mercy Mgongolwa, wa pili kutoka kushoto, akimkabidhi kompyuta nane Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mbeya, Nyasenga Enock kwa ajili ya kuzigawa kwa Halmashauri nne za Mkoa huo wa Mbeya. Wa kwanza kushoto ni Meneja wa Kanda ya Kusini wa Bayport Financial Services, Emmanuel Nzuttu. Wa pili kutoka kulia ni Meneja wa Bayport Mbeya, Mohamed Kisoki akifuatiwa na wakala wake Kurwa Lighton. Picha na Mpiga Picha wetu Mbeya.

Na Mwandishi Wetu,Mbeya
SERIKALI ya Mkoa wa Mbeya, zimewataka watumishi wa umma katika mkoa wao,hususan kupitia ofisi zitakazonufaika na msaada wa kompyuta nane kutoka kwenye taasisi ya kifedha ya Bayport Financial Services, kuongeza ufanisi wa kazi kwa kupitia vitendea kazi hivyo vilivyotolewa.

Hayo yamesemwa mwishoni mwa wiki na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa Mbeya, Nyasenga Enock, akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Mheshimiwa Amos Makalla, kwenye makabidhiano ya kompyuta zilizotolewa na Bayport kwa ajili ya ofisi ya Halmashauri ya Tunduma, Ileje, Mbeya na Rungwe, huku kila ofisi ikipokea kompyuta mbili.
Majadiliano yakiendelea katika makabidhiano hayo ya kompyuta kutoka Bayport Financial Services mwishoni mwa wiki, mkoani Mbeya.

Akizungumzia hilo, Enock alisema kwamba haitakuwa na maana kama msaada wa kompyuta za Bayport hautaongeza ufanisi kazini na kutoa huduma bora kwa wananchi kwa kutumia vyema vitendea kazi hivyo vipya vinavyoweza kuleta tija kama kila mtumishi atafanya kazi kwa nguvu zote ili kuwatumikia wananchi.
Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Mbeya, Nyasenga Enock akigawa kompyuta hizo kwa wahusika baada ya kukabidhiwa na Bayport Financial Services.


Previous
Next Post »