Rais
Mteule wa Marekani, Donald Trump anagharimikiwa na jiji la New York
kiasi cha shilingi milioni moja dola za kimarekani kwa siku kutokana na
ulinzi wa Polisi, kwa mujibu maofisa kadhaa wa jiji hilo na vyanzo hivyo
vinasema gharama hizo haziwezi kushuka kutoka hapo nyumbani kwake kwa
sasa.
Shirika
la habari la CCN, limeripoti kwamba “kila rais anapaswa kuwa na ulinzi
wa kisheria pindi anapomaliza muhula wake wa utumishi,” lakini ulinzi
kwa Trump ni gharama maradufu kwa kuwa anaishi kati kati ya mji maarufu,
Watoto
wa Trump na wajukuu zake wote kwa pamoja wanapata ulinzi wa kitaifa na
itifaki zote na mke wake Melania na mtoto wake mdogo Barron anapanga
kubaki jiji New York mpaka mwisho wa muhula wake wa shule, gharama
zitabaki kuwa juu zaidi.
Trump
mwenyewe ameweka wazi kwamba anapendelea kuendelea kufanya kazi kutokea
katika jiji la New York kama ikiwezekana ambapo itaulazimu mji huo
kuweka katika hali ya ulinzi wa kisheria zaidi,”amesema Meya wa Jiji
hilo la New York, Bill de Blasio katika mkutano na vyombo vya habari
ijumaa iliyopita.
Cha
msingi hapa ni ulinzi na usalama, “ ni ulinzi kwa ajili ya rais mteule,
familia yake na wasaidizi wake wote,” amesema de Blasio, kwa mujibu wa
CNN, “ Hatujawahi kuwa na rais wa Marekani anaishi maeneo haya ya New
York, au kuwa na kiongozi wa nchini anakuwa maeneo kila wakati,”
Sign up here with your email