LIPUMBA APINGA KESI YA CUF , BODI YA WADHAMINI YAMWOMBA JAJI KUJI KUJIONDOA KUISIMAMIA. - Rhevan Media

LIPUMBA APINGA KESI YA CUF , BODI YA WADHAMINI YAMWOMBA JAJI KUJI KUJIONDOA KUISIMAMIA.


lipumba
Novemba 24, 2016 imetajwa tarehe ya kesi ya Bodi ya Wadhamini ya Chama cha Wananchi (CUF) dhidi ya Msajili wa Vyama vya Siasa Jaji Fransic Mutungi, Mwanasheria Mkuu wa Serikali na aliyekuwa mwenyekiti wa CUF Prof. ibrahim Lipumba pamoja na watu 11 waliokuwa wanachama wa chama hicho ambayo itasikilizwa Disemba 6, 2016.
Upande wa wadaiwa wamejibu maombi ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, pamoja na kuipinga kesi hiyo dhidi yao.
Wakili upande wa wadai ambao ni Bodi ya Wadhamini CUF, Juma Nassoro amesema Mwanasheria Mkuu, Msajili wa Vyama vya Siasa na Prof. Lipumba pamoja na wenzake wameweka kila mmoja ameweka mapingamizi kwa kutumia hoja mbalimbali ikiwemo kuwa, Mahakama hiyo haikutoa kibali cha kufunguliwa kwa shauri hilo.
“Upande wa wajibu maombi akiwemo msajili, mwanasheria na Lipumba walijibu maombi Novemba 17 na sisi tumejibu. Lakini pia kila upande umeweka mapingamizi kwa hoja kadhaa ikiwemo kuwa
Mahakama Kuu Kanda ya DSM haijatoa kibali cha kufungua shauri hili na kwamba sisi baada ya kusoma hoja zao tumeona ni hoja za kupikwa hivyo tumeweka kipingamizi,” amesema.
Aidha, Wakili Nassoro amesema Bodi ya Wadhamini imemuomba Jaji Amma-Isario Munisi anayeendesha kesi hiyo kujiondoa kutokana na sababu mbalimbali ambazo hakuzitaja kwamba barua ya maombi haijamfikia jaji huyo rasmi.
“Wadhamini wameomba jaji kujiondoa ili asiendelee kuendesha kesi hiyo ingawa barua ya maombi haikuingia kwenye faili. Sababu za wadhamini kumtaka jaji kujiondoa zipo sitazisema sababu hiyo barua haijamfikia,” amesema.
Amesema tarehe ya siku ya kusikilizwa kesi itakapofika kitakachojadiliwa ni ombi la wadhamini la kumtaka jaji kujiondoa na mapingamizi yaliyowekwa na pande zote mbili.
Nassoro amesema kuwa ” Nimefungua mashtaka kwa niaba ya chama
Kama hakutakuwa na nguvu ya ndani, ushindi uko wazi sababu tunavithibitisho na madai yetu ni ya msingi na wadaiwa wao wana vitu vya kupikwa. Kuhusu jaji kukataliwa ni jambo la kawaida katika kesi kama hizi.”
Previous
Next Post »