NYOKA MKUBWA ZAIDI DUNIANI AFARIKI DUNIA. - Rhevan Media

NYOKA MKUBWA ZAIDI DUNIANI AFARIKI DUNIA.

Image captionJoka kubwa zaidi kuwahi kukamatwa duniani amekufa.
Joka kubwa zaidi kuwahi kukamatwa duniani amekufa.
Chatu huyo aliyepatikana katika eneo lililokuwa likijengwa nchini Malaysia karibu na mti mkubwa uliokatwa katika kisiwa cha Penang.
Joka hilo linakisiwa kuwa takriban mita 8 hivi sawa na futi 26 lilipatikana siku ya Alhamisi iliyopita.
Kwa bahati mbaya joka hilo lilikufa jumapili lilipokuwa likizaa.
Image captionChatu huyo aliyepatikana katika eneo lililokuwa likijengwa nchini Malaysia
Afisa anayesimamia ujenzi katika kisiwa hicho cha Penang, Herme Herisyam aliiambia BBC.
Kulingana na daftari za kumbukumbu za Guinness, joka anayeshikilia rekodi ya dunia anaurefu wa mita 7.67.
Chatu huyo anayeitwa Medusa ana uzani wa kilo 158 na anaishi katika jumba moja mjini Kansas City, Missouri Marekani.
Image captionBw Herisyan anasema kuwa alikuwa na uzani wa kilo 250.
Hata hivyo joka huyo wa Malaysia ambaye alikuwa mkubwa zaidi yake hakuwa amepimwa na kuthibitishwa kuwa mrefu zaidi kabla ya kufa kwake.
Bw Herisyan anasema kuwa alikuwa na uzani wa kilo 250.
Hata hivyo katika harakati za kumuokoa kutoka maficho yake inakisiwa kuwa aliumia na hivyo akafa kabla hajafikishwa kwenye hifadhi ya wanyama alikotarajiwa kutuzwa hadi ajifungue.
Previous
Next Post »