MKUU WA MKOA AFUTA UONGOZI WOTE WA KIJIJI NA KUFANYA MAAJABU YA MWAKA. - Rhevan Media

MKUU WA MKOA AFUTA UONGOZI WOTE WA KIJIJI NA KUFANYA MAAJABU YA MWAKA.

Siku cha chache tu baada wanawake wawili vikongwe kuuawa    kinyama kwa imani za ushirikina katika kijiji cha Kenyamusana    wilayani Rorya,serikali mkoani Mara imeufuta uongozi wote wa    serikali ya kijiji hicho ikiwa ni pamoja kumsimamisha kazi     Afisa Mtendaji wa kata ya Baraki kwa madai ya kushindwa kuzuia   mauaji hayo ya kikatili.
Mkuu wa Mkoa wa Mara Bw Magesa Mulongo,amechukua uamuzi huo baada ya kufika katika kijiji hicho na kusema kuwa mipango ya mauaji   ya wanawake hao vikongwe imefanyika mchana kweupe lakini   viongizi hao kijiji na kata walishindwa kuchukua hatua za     kuzuia mauaji hayo kabla ya kutokea.
 
kiongozi huo ambaye pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Ulinzi na    Usalama wa mkoa wa Mara,ameliagiza jeshi kufanya uchunguzi wa  haraka na kuhakikisha watu wote walihusika kufanya mauaji hayo  ya  kinyama wanakamatwa na kufikishwa katika vyombo vya sheria.
 
Naye Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalum ya Tarime na Rorya   Kamishina Msaidizi wa Jeshi la Polisi ACP Andrew Satta,amesema    tayari watu 14 wamekamatwa kuhusiana na tukio hilo huku    akiwataka watu wote waliohusika kufanya unyama huo      kujisalimisha wenyewe.
 
Wiki iliyopita kundi la watu katika kijiji hicho waliwaua kwa   kuwakata mapanga kisha kuwachoma moto wanawake wawili vikongwe kwa tuhumu za kujihusisha na ushirikina,tukio ambalo limesababisha hofu kubwa kwa wanawake wengi wenye umrimkubwa katika kijiji hicho.
Previous
Next Post »