MONDULI KUNUFAIKA NA MRADI WA KUHIMILI MABADILIKO YA TABIA NCHI - Rhevan Media

MONDULI KUNUFAIKA NA MRADI WA KUHIMILI MABADILIKO YA TABIA NCHI

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais
Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira )January Makamba 

Arusha.Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira )January Makamba amesema Monduli ni moja ya wilaya zitakazonufaika na mradi wa kuhimili mabadiliko ya tabia  nchi ili kuwasaidia wafugaji wanaohamahama na kusababisha uharibifu wa mazingira.
Monduli ni moja ya wilaya zinazokumbwa na ukame hali inayosababisha wakazi wa eneo hilo ambao  kwa  asilimia kubwa ni   jamii ya wafugaji  kuhama kutoka sehemu hadi nyingine kutafuta malisho.
Amesema  mradi huo utasaidia kwa kiasi kikubwa wafugaji kupata malisho bora kwa ajili ya mifugo yao ili kupunguza changamoto ya kuhama hama.
Makamba amesema hayo leo wakati akipokea taarifa ya hali ya mazingira katika wilaya ya Monduli alipokwenda kukagua shughuli za uhifadhi wa mazingira katika ziara yake ya mikoa mbalimbali


Previous
Next Post »