MAMBO YAANZA KUWANYOOKEA WAMILIKI WA MALORI - Rhevan Media

MAMBO YAANZA KUWANYOOKEA WAMILIKI WA MALORI


Dar es Salaam. Wamiliki wa malori nchini wamesema matumaini ya kupata kazi yameanza kuonekana baada ya kuongezeka mizigo ya kusafirisha nje ya nchi, inayopitia Bandari ya Dar es Salaam.
Wamiliki hao na wasafirishaji wengine mwaka jana walikuwa wakilalamika kukosekana kwa mizigo katika Bandari ya Dar es Salaam na wengine kulazimika kuyaegesha malori yao.
Akizungumza jana na gazeti hili, Mjumbe wa Bodi ya Chama cha Wamiliki wa Malori Tanzania (Tatoa), Rahim Dosa alisema, “tunaanza kuona matumaini mbele yetu.”
Alisema wameanza kupata mizigo ingawa hali bado si shwari, lakini imeanza kuongezeka kuanzia Desemba  mwaka jana na Januari mwaka huu.
“Tunaomba Mungu hali hii iendelee ili tuweze kufanya biashara kama ilivyokuwa zamani,” alisema.
Katibu Mkuu wa Chama cha Wasafirishaji wa Mizigo Bandarini (Taffa), Tony Swai alisema mizigo bandarini imeanza kuongezeka.

Previous
Next Post »