ELIMU BURE YAONGEZA UDAHILI WA WANAFUNZI SHULE ZA MSINGI - Rhevan Media

ELIMU BURE YAONGEZA UDAHILI WA WANAFUNZI SHULE ZA MSINGI

MUS


ELIMU bure yaongeza idadi ya udahili wa wanafunzi wa shule za msingi nchini waongezeka kutoka 1,282,000 mwaka 2015 hadi kufikia 1,896,000 mwaka 2016 ambayo ni sawa na ongezeko la asilimia 84.5.
Hayo yamebainishwa na Katibu Mkuu wa Ofisi ya Rais –Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhandisi Mussa Iyombe alipokuwa anaongea katika kipindi cha tunatekeleza kinachoratibiwa na Idara ya Habari – MAELEZO na kurushwa na Televisheni ya Taifa (TBC1) jana jijini Dar es Salaam.
Mhandisi Mussa Iyombe amesema kuwa dhamira ya Serikali nikuhakikisha inatoa huduma bora za kijamii ikiwemo elimu, afya, miundombinu na maji safi.
“Dhamira ya Serikali ni kutoa huduma bora za afya,elimu,maji na miundombinu ndiyo maana Serikali ya Awamu ya Tano ikaja na Sera ya Elimu bure ili kutoa fursa kwa wananchi wake kupata elimu,”alisema Mhandisi Iyombe.
Aidha Muhandisi Iyombe amebainisha kuwa kazi kubwa ya TAMISEMI ni kuratibu na kusimamia Mikoa, Wilaya na Halmashauri katika utoaji wa huduma bora za maendeleo kwa wananchi.
Aliongeza kuwa ili Serikali iweze kutimiza azma yake ya kuwapatia huduma za maendeleo wananchi wake imeweka mfumo dhatibiti wa ukusanyaji wa mapato katika halmashauri nchini ili kuhakikisha fedha inapatika kiwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo.
Mhandisi Iyombe amesema kuwa mapato yanayokusanywa na halmashauri nchini ni kwa ajili ya kutoa huduma za kimaendeleo ili wananchi wanufaike.
Previous
Next Post »