Tanzania imezidi kudidimia chini katika viwango vya soka Duniani ambavyo hutolewa na shirikisho la soka ulimwenguni FIFA.
Kwa sasa Tanzania ipo nafasi ya
160 Duniani ikiwa imeshuka kwa nafasi 16 baada ya awali kuwa katika
nafasi ya 144 kabla ya mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Zimbabwe
uliopigwa Harare Novemba 13 mwaka huu.
Tanzania ilipoteza kwa magoli 3-0
dhidi ya Zimbabwe mchezo ambao ulikuwa unatambuliwa na kalenda ya FIFA
na moja kwa moja hii ndiyo sababu kubwa ya Tanzania kuendelea kudidimia
chini kwenye viwango hivyo vya ubora wa soka Duniani.
Barani Afrika, Tanzania inakamata nafasi ya 48 huku Argentina ikiendelea kuongoza viwango hivyo vya Dunia
Sign up here with your email