MAREKANI YASHAMBULIA NGOME ZA IS LIBYA. - Rhevan Media

MAREKANI YASHAMBULIA NGOME ZA IS LIBYA.

Shambulio la Marekani nchini Libya
Marekani imefanya mashambulio ya angani katika ngome za wapiganaji wa Islamic State nchini Libya kufuatia ombi la serikali ya taifa hilo inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa,Pentagon imesema.
Mashambulio hayo yalilenga ngome za kundi hilo zilizopo katika bandari ya Sirte.
Waziri mkuu wa Libya Fayez al Sarraj katika hotuba ya runinga,amesema kuwa mashambulio hayo yalisababisha 'hasara kubwa'.
Shambulio la Marekani
Mataifa ya Magharibi yana wasiwasi mkubwa kuhusu ukuaji wa kundi hilo nchini Libya.
Mashambulio hayo ni ya kwanza yaliofanywa na Marekani yakipangwa na serikali ya Libya.
Previous
Next Post »