KAMPUNI ya Yono Auction Mart ya jijini Dar-es-salaam,imewatoa nje  kwa nguvu wanunuzi na wapangaji wa nyumba za serikali mkoani Singida, kwa kile kilichodaiwa kuwa  hawajamaliza kulipa madeni yao kwa wakati.
Wadaiwa sugu watatu waliokuwa na mikataba ya kununua nyumba TBA/SGD/GOVT/BDG/LC/VETA namba moja,mbili na tatu zilizoko katika maeneo ya VETA mjini humo, wanadaiwa zaidi ya shilingi 20.9 milioni.
Mpangaji mmoja ambaye amepanga nyumba namba TBA/SGD/BDG/SAB/9 iliyopo maeneo ya saba saba mjini humo, anadaiwa shilingi 179,000.00.
Meneja wa kampuni ya Yono tawi la Dodoma, Tatu Rashidi,alisema zoezi hilo la kuwaondoa kwa nguvu wadaiwa sugu wa nyumba za serikali,linaendelea kufanywa na kampuni ya Yona nchi nzima.Kazi hiyo wamekabidhiwa na Wakala wa majengo Tanzania (TBA).
Meneja wa kampuni ya Yono Auction Mart tawi la Dodoma,Tatu Rashidi
Meneja wa kampuni ya Yono Auction Mart tawi la Dodoma,Tatu Rashidi,akizungumza na waandishi wa habari  (hawapo pichani) juu ya zoezi la kuwatoa kwa nguvu wadaiwa sugu wa nyumba za wakala wa majengo Tanzania (TBA) mkoani Singida. Jumla ya watu watatu wenye mikataba ya kununua nyumba hizo,wametolewa kwa nguvu kwenye nyumba zao zilizopo maeneo ya VETA,kwa kushindwa kulipa madeni yao yanayofikia zaidi ya shilingi milioni 20.
 “Kazi hii ambayo ni endelevu,tumeianzia katika mkoa wa Dodoma na sasa tupo mkoa wa Singida, tukimaliza, tunahamia mkoa wa Manyara. Lengo letu ni kwamba watu walioingia mkataba wa kununua nyumba za serikali, wanamaliza kulipa madeni yao.Hali kadhalika na wale waliopanga nyumba za serikali, wamalize kulipa madeni ya pango”,alifafanua Tatu.
Alisema wadaiwa sugu hao wanaotolewa kwa nguvu kwenye nyumba za serikali, wakilipa madeni yao ndani ya siku 14,watakabidhiwa nyumba zao.
“Watakoshindwa kulipa ndani ya muda huo,kampuni ya Yono itabidi kuuza kwa njia ya mnada vyombo/mali zao ambazo tunavishikilia kwa sasa”,alisema.
Fundi seremala akifunja mlango wa nyumba no.TBASGDBDGSAB9 iliyopo maeneo ya saba saba ambayo mpangaji wake anadaiwa shilingi 197,000.00
Fundi seremala akivunja mlango wa nyumba no.TBA/SGD/BDG/SAB/9 iliyopo maeneo ya saba saba ambayo mpangaji wake anadaiwa shilingi 197,000.00.
Kwa upande wake Afisa wa wakala wa majengo Tanzania (TBA) mkoa wa Singida, Mohammed Mloka,alisema wateja walioingia mkataba wa kununua nyumba za serikali,wanapaswa kuheshimu masharti ya mikataba yao,ili kuondokana na aibu na usumbufu wa kutolewa kwa nguvu kwenye nyumba hizo.
Mloka alitumia fursa hiyo kuwataka wapangaji na walionunua nyumba za serikali,kujenga utamaduni wa kulipa kodi na madeni ya ununuzi wa nyumba hizo kabla ya kufikiwa na mkono wa Yono.
Imedaiwa kwamba kampuni ya Yono, imepewa orodha ya nyumba zaidi ya 3,000 nchi nzima za walionunua na wengine waliopangisha nyumba za wakala wa majengo,ambao muda wa kulipa madeni,uliishapita.
Operation Manager wa kampuni ya Yono Auction Mart ya jijini Dar (kulia) akitoa vitu vya wadaiwa sugu singida
Meneja Uendeshaji wa kampuni ya Yono Auction Mart ya jijini Dar-es-salaam, Atukuzwe Mhugo,akishiriki zoezi la kuwatoa nje kwa nguvu wadaiwa sugu wa nyumba za wakala wa majengo Tanzania (TBA) za mjini Singida.
Vijana wakishiriki kutoa vyombo kwenye nyumba ya wakala wa majengo Tanzania (TBA)
Vijana wakishiriki kutoa vyombo kwenye nyumba ya wakala wa majengo Tanzania (TBA) TBA/SGD/BDG/SAB/9 baada ya mpangaji wake kushindwa kulipa deni la shilingi 197,000.00.(Picha na Nathaniel Limu).