Mashindano ya Maisha Plus ambayo yamefahamika kwa kuwa na uhalisia zaidi yamerudi katika awamu nyingine tena.
Msimu huu mpya tutegemee ushindani mkubwa zaidi kutokana na wigo wa mashindano hayo kuwa kujikita katika nchi 5 za Afrika Mashariki ambazo ni Kenya,Uganda,Rwanda,Burudi na wenyeji Tanzania.
Maisha Plus 2016 itakuwa inaruka katika runinga ya Azam Two kuanzia saa 3:00 usiku mpaka saa 4:00 usiku Na usahili ulianza June 4, mkoani Mtwara.
Mashindano hayo msimu huu yamekuja na donge nono kwa mshindi kwani atajinyakulia kitita cha shilingi za kitanzania milioni 30.
Sign up here with your email
