WAZIRI AZUNGUMZA NA RAIS WA MAHAKAMA YA KIMATAIFA. - Rhevan Media

WAZIRI AZUNGUMZA NA RAIS WA MAHAKAMA YA KIMATAIFA.




Waziri wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na Kimataifa, Mhe. Balozi Dkt. Augustine Mahiga akizungumza na Rais wa Mahakama ya Kimataifa ya Masalia ya kesi za Mauaji ya Kimbari ya Rwanda (Mechanism for International Criminal Tribunals-(MICT) inayojengwa katika eneo la Lakilaki jijini Arusha, Mhe. Theodor Meron.

Rais huyo alifika Wizarani kwa ajili ya kujitambulisha kwa Mhe. Waziri, kumweleza maendeleo ya ujenzi wa Mahakama hiyo pamoja na kuishukuru Serikali ya Tanzania kwa ushirikiano na mchango mkubwa inaotoa katika kufanikisha ujenzi huo. Pia aliipongeza Tanzania kwa kuwa mstari wa mbele katika kusimamia utawala wa sheria na haki.
Sehemu ya ujumbe uliofuatana na Mhe. Meron, Rais wa MICT.
Picha ya pamoja
Mhe. Mahiga na Mhe. Meron


Mhe. Mahiga akiagana na Mhe. Meron

Previous
Next Post »