WARSHA YA MAJI KUSINI MWA JAGWA LA SAHARA YAFANYIKA MKOANI IRINGA. - Rhevan Media

WARSHA YA MAJI KUSINI MWA JAGWA LA SAHARA YAFANYIKA MKOANI IRINGA.



 Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Iringa Bwana Richard Kasesela leo (jana) amefungua Warsha ya mwanzo wa mradi wa utafiti wa "HALI YA MAJI CHINI YA ARDHI KATIKA AFRIKA, KUSINI MWA JANGWA LA SAHARA" katika hotel ya Gentle Hill. Mradi huu unafanywa na chuo kikuu SUA na Gro `Futures.

Akizungumza katika hotuba yake alisema;Matumizi ya maji chini ya ardhi yamekua kwa kasi zaidi hivi karibuni kutokana na maendeleo ya maarifa ya elimu ya sayansi. Changamoto kubwa ni udhibiti wa rasilimali hii chini ya ardhi haujaenda sambamba na  ongezeko hili la mtaumizi. Hivyo basi utafiti huu utasaidia kutengeneza utaratibu thabiti wa matumizi ya maji yaliyo chini ya ardhi.

Uchumi wa nchi ya Tanzania kiasi kikubwa unategemea uwepo wa maji, utunzaji na mipango thabiti itasaidia Tanzania kusonga mbele. Umefika wakati sasa kwa nguvu zote tusimamie maji tuliyo nayo kwa kuwa na mkakati wa pamoja wa maji yaliyo juu ya ardhi na yale ya ardhini. 
Nampongeza sana Prof Japhet Kashaigili ambaye ndie mtafiti Mkuu pamoja na Prof Richard Taylor Mtafiti mwandamizi kwa kuchagua Iringa kuwa kituo cha utafiti naamini mkoa utanufaika si tu na matokeo ya utafiti bali pia baadhi ya wana sayansi wetu kushiriki kwenye utafiti."

 Wadau wa Warsha hiyo wakimsikiliza  Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Iringa Bwana Richard Kasesela (hayupo pichani) alipokuwa akizungumza
  Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Iringa Bwana Richard Kasesela pichani kati akiwa na Prof Japhet Kashaigili ambaye ndie mtafiti Mkuu pamoja na Prof Richard Taylor Mtafiti mwandamizi
wakiwa katika picha ya pamoja na Wadau wengine wa Warsha hiyo

Previous
Next Post »