Mgombea wa Nafasi ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Bw. Igor Luksic
( Montenegro), akimwaga sera zake mbele ya wajumbe wa Baraza Kuu la
Umoja wa Mataifa, wakati wa majadiliano/mhadalo usio rasmi
ulioandaliwa na Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kwa lengo kutoa
fursa kwa wanaowania nafasi ya Katibu mkuu kueleza sera zao na kisha
kuulizwa maswali
Bi. Irina Bokova ( Burgalia) mmoja wa wanawake wanne waliojitokeza hadi
sasa kuwania nafasi ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa naye akijieleza
mbele ya wajumbe wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.
Bw. Antonio Guterres ( Portugal) mmoja wa wagombea waliohojiwa
katika siku ya kwanza ya mdahalo usio rasmi wa kuwasikiliza wagombea
waliojitokeza kuwaania nafasi itakayoachwa wazi na Ban Ki Moon, mwishoni
mwa mwaka huu. jumla ya wagombe tisa wamekwisha jitokeza mpaka jana (
jumanne).
Taswira ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, katika siku ya kwanza ya
mdahalo wa kihistoria ya wagombea nafasi ya Ukatibu Mkuu wa Umoja wa
Mataifa, Mdahalo/majadiliano ya kwanza ya aina yake kufanyika katika
nafasi ya kumtafuta Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa .
Na Mwandishi Maalum,
New York
Baraza Kuu la Umoja
wa Mataifa, jana ( Jumanne) limeandika
historia kwa mara nyingine, kwa kuanza
mchakato usio rasmi wa kuwasikiliza na kuwauliza maswali wagombea watarajiwa waliojitokeza kuwania nafasi ya
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.
Mchakato huo ulianza
kwa kuwasikiliza wagombea watatu kati ya tisa wakiwamo wanawake wake wanne ambao hadi siku ya jumanne walikuwa wametangazwa
rasmi kuwania nafasi hiyo itakayo achwa wazi na Katibu Mkuu wa sasa Ban Ki Moon anayemaliza muda wake mwishoni mwa mwaka huu.
Katika awamu ya hiyo
ya kwanza, kila mgombea mtarajiwa alipewa fursa ya kujieleza na kuelezea
visheni yake, sera, mipango, vipaumbele
vyake na nini anatarajia kukifanya endapo
atachaguliwa kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa
, Umoja wenye wanachama 193.
Walioshiriki mdahalo
huo katika siku ya kwanza walikuwa ni Dr. Igor Luksic ( Motenegro), Bi. Irina
Bokova ( Bulgaria) na Bw. Antonio
Guterres ( Portugal)
Wengine ambao
wamejitokea kuwania nafasi hiyo ni Dr.
Damilo Turk ( Slovenia) Prof.Dr. Vesna Pusic ( Crotia), Bi. Natalia Gherman (
Moldova), Dr. Srgian Kerim ( Macedonia),
Bi. Helen Clark ( New Zeland) na
Bw. Vuk Jeremic ( Serbia)
Ulikuwa ni mdahalo wa
aina yake wa kwanza kutokea tangu kuanzishwa kwa Umoja wa Mataifa miaka karibu 70
iliyopita, mdahalo ulioendedeshwa
katika mazingira ya uwazi, na ambao kwayo
umebadilisha kabisa utaratibu wa kumpata Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa.
Sign up here with your email