SAFARI YA NDEGE YAKATIZWA KUTOA SALAMU ZA MWISHO. - Rhevan Media

SAFARI YA NDEGE YAKATIZWA KUTOA SALAMU ZA MWISHO.

Image copyright
Image captionSafari ya ndege yakatizwa kutoa salamu za mwisho
Safari ya ndege iliyokuwa ikitokea uwanja wa ndege wa Manchester ilikatizwa ilikuruhusu babu mmoja na mkewe kutoa salamu za mwisho kwa mjukuu wao aliyekuwa akipumua hewa yake ya mwisho hospitalini huko Uingereza.
Babu na mkewe walikuwa safarini kuelekea Australia kwa likizo walipopokea ujumbe mfupi wa simu kutoka kwa jamaa yao akisema kuwa mjukuu wao alikuwa na saa chache tu za kuishi.
Habari hizo za kushtua sana ziliponza bibi huyo ambaye alimueleza mhudumu wa ndege hiyo.
Kwa sababu ya huzuni na kububujikwa kwa huruma kutoka kwa abiria wenzake, mhudumu mmoja alikwenda na kumpasha habari hizo rubani wa ndege hiyo ya Etihad.
Image copyrightREUTERS
Image captionNdege hiyo ya Eihad ilikuwa ikielekea Abu Dhabi
Kwa mshangao rubani huyo alipunguza kasi ya ndege hiyo na kuomba ruhusa kurejea katika eneo la kuegesha ndege ilikuwapa fursa kushuka na kuelekea hospitalini kumuaga mjukuu wao.
Japo shughuli hiyo ya kuwashusha na kupakua mizigo yao ilisababisha ndege hiyo na abiria wengine kuchelewa, juhudi hiyo ya kipekee ya rubani huyo wa Etihad ilimsababishia kusifiwa na abiria na wapanga safari katika uwanja huo wa ndege.
Previous
Next Post »