MBUNGE WA CHADEMA MATIKO AMUUNGA MKONO RAIS MAGUFULI. - Rhevan Media

MBUNGE WA CHADEMA MATIKO AMUUNGA MKONO RAIS MAGUFULI.

MBUNGE wa Tarime Mjini kupitia Chadema, Esther Matiko, amepongeza Rais Dk. John Magufuli kwa kupambana na rushwa na ubadhirifu wa mali ya umma, ambavyo amesema vilikuwa tishio kwa ustawi wa taifa.

Akzungumza juzi katika uwanja wa mpira wa Sabasaba mjini hapa, Matiku alisema rushwa, ufisadi, ukwepaji kodi na watumishi hewa vilikithiri na kusababisha wananchi kuishi maisha magumu.
Katika mkutano huo ambao Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi, mwigulu nchemba alikuwapo, Matiku alisema kasi ya kupambana na maovu mbalimbali serikali, maarufu kama utumbuaji majipu, imeleta matumaini mapya kwa Watanzania.
Alisema rushwa, ubadhirifu, ukwepaji kodi na wafanyakazi hewa vilisababisha kupotea kwa fedha nyingi na kusababisha miradi mingi ya maendeleo kukwama.
“Suala hili si la kiitikadi bali linapaswa kupongezwa na kila Mtanzania mwenye mapenzi mema na taifa hili. Kasi hii iendelee hadi maeneo ya vijijini ambako pia kuna matatizo,” alisema.
Sambamba na kupongeza kasi hiyo ya Rais Magufuli, Matiko alimwomba Waziri Nchemba kuagiza kujengwa kwa mnada wa ng’ombe wa Magena, kilomita nne ktoka Tarime mjini, barabara ya Sirari badala ya kujengwa Kirumi,wilayani Rorya, ambako mnada huo ulikuwako tangu awali.
Alisema ujenzi wa mnada huo katika eneo la Magena, utaisaidia Halmashauri ya Mji Tarime, ambayo haina vyanzo vingi vya mapato. Alisema kujengwa kwa mnada huo kwenye eneo hilo,utawezesha kuvuka lengo kwa asilimia 80, hivyo kuinusuru kufutwa.
Matiko alisema mgawanyo wa halmashauri kwa kuigawa halmashauri ya wilaya ya Tarime na kuundwa ile ya Mji wa Tarime, kulisababisha kupatikana kwa kata nane ambazo alisema hazina vyanzo vya mapato.
“baada ya kugawanywa, halmashauiri ya mji haina vyanzo vya uhakika wa mapato tofsuti na ile ya wilaya ya Tarime, ambayo ina vyanzo vingi, kikiwamo cha mgodi wa North Mara, ulioko Nyamongo ambao unamilikiwa na kampuni ya madini ya Acacia.
“Ninakuomba Mheshimiwa Waziri usikie kilio changu na cha wana- Tarime Kuhusu ujenzi wa mnada wa ngo'mbe katika kijiji cha Magena badala ya Kujengwa Kirumi.
Nawaomba wahisani kuja wilayani Tarime kujenga viwanda vikiwamo vya biskuti kwani kuna viazi na ndizi kwa wingi katika wilaya yetu hii kwani mavuno ni mara mbili kwa mwaka,” alisema Matiko.
Waziri Nchemba kwa upande wake alisema amepokea kilio hicho cha Mbunge na kwamba atafikisha maombo yake ngazi husika na kuyafanyia kazi.
“Ujenzi waviwanda vikiwamo vya ngozi na biskuti ni suala zuri na kwa maendeleo yawananchi wetu. Nimepokea maombi haya na nitayafanyia kazi,” alisema.
Previous
Next Post »