MAPIGANO MAKALI KATIKA LA NAGORNO-KARABAKH YANAENDELEA. - Rhevan Media

MAPIGANO MAKALI KATIKA LA NAGORNO-KARABAKH YANAENDELEA.

2a63824090474700a094ad8225732b67_18

Azerbaijan  na  majeshi  yanayotaka  kujitenga  katika  eneo la Nagorno – Karabakh  yamekubaliana  kusitisha mapigano  kuanzia leo kufuatia  siku  kadhaa  za mapigano  makali  katika  jimbo  hilo linaloleta  mvutano tangu  mwaka  1994.
Wizara  ya  ulinzi   ya  Azerbaijan  imesema  operesheni  ya majeshi  ya  Azerbaijan  na  Karabakh  zimesitishwa.
Msemaji wa  wizara  ya  ulinzi  katika  jimbo  lililojitangazia uhuru  la  Nagorno Karabakh  amethibitisha  usitishaji  huo wa  mapigano  mapema  leo.
Mapigano hayo yalizuka mwishoni  mwa  juma ambapo  kila  upande  ukilalamikia upande  mwingine  kwa  kuchochea na  matumizi  ya silaha  nzito.
Previous
Next Post »