GWAJIMA ARUDISHWA TENA MAHAKAMANI, - Rhevan Media

GWAJIMA ARUDISHWA TENA MAHAKAMANI,


April 6 mwaka huu, mkuu wa mkoa wa Arusha mh. Daud Felix Ntibenda alitoa amri ya kuyadhibiti makanisa ya kilokole jijini Arusha kwa madai kuwa yanawasumbua wananchi kwa kupiga vinanda na kuimba usiku kucha.

Ntibenda alitoa  amri  hiyo  ofisini kwake   wakati akizungumza na wenyeviti wa serikali za mitaa na watendaji wa mitaa yote ya jiji la Arusha.

Alisema hataweza kuvumilia makanisa hayo kuzinduliwa kila mahali katika makazi ya watu na kufanya ibada usiku kucha.

"Mimi ni mkristo, sikatazi waumini kusali, lakini nataka kuwe na utaratibu maalumu, sio kila kukicha unakuta kanisa jipya na kibaya zaidi yanasumbua hata wageni wanaoingia jijini hapa." Alisema Ntibenda.

Kutokana na kauli hiyo ya mkuu wa mkoa, Askofu Mkuu wa Kanisa na Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima  amejitokeza hadharani kupinga kauli hiyo huku akihoji kuna baa ngapi mitaani zinazopiga kelele kushinda hata makanisa ya kilokole.

Gwajima amesema Tanzania ni nchi huru, na kwa mujibu wa Katiba ya Tanzania, kila mtu ana haki ya kuabudu muda wowote na wakati wowote atakao bila kuingiliwa na mtu yeyote.

Amesema waumini wa makanisa ya kilokole Tanzania wako zaidi ya milioni 11, hivyo kuwazuia kuabudu ni sawa na kutafuta matatizo mengine.

Gwajima  amesema waumini wa Kiislam huamka saa kumi usiku kuswali kwa sauti kubwa na hakuna mtu huwaingilia kwa  sababu  hiyo ni haki yao kikatiba.

Previous
Next Post »