Mahakama ya Hakimu mkazi Arusha imempa dhamana Mtuhumiwa Isaac Abakuki anayetuhumiwa kumtukana Rais John Magufuli kupitia kwenye ukurasa wake kwenye mtandao wa kijamii wa Facebook.
Hakimu mfawidhi Agustino Rwezire amesema Mahakama baada ya kupitia hoja mbili zilizotolewa na upande wa mashtaka na mshtakiwa, imeridhia kutoa dhamana kama haki ya msingi ya mshtakiwa kutokana na kosa alilotenda ambapo dhamana hiyo ni ya Wadhamini wawili waliotakiwa kuwa na jumla ya shilingi milioni tano.
Sign up here with your email