
Rais wa Uganda Yoweri Museveni amesema uchaguzi uliofanyika nchini humo Alhamisi wiki iliyopita ulikuwa wa haki na akasema wanaoutilia shaka “hawaielewi Uganda.”
Aidha, ametetea hatua ya maafisa wa usalama kumzuilia mgombea mkuu wa upinzani Dkt Kizza Besigye wa chama cha FDC.
Tume ya Uchaguzi ilisema Jumapili kwamba Bw Museveni alipata ushindi wa asilimia 60.75 dhidi ya mpinzani wake wa karibu Dkt Besigye aliyepata asilimia 37.35.
Upinzani umedai kuwepo wizi wa kura na waangalizi wa kimataifa wamesema pia kwamba hakukuwa na nafasi sawa ya ushindani.
Waangalizi hao wamelalamikia kukamatwa na kuzuiliwa kwa Dkt Besigye, kucheleweshwa kwa kufunguliwa kwa vituo vya kupigia kura na kuzimwa kwa mitandao ya kijamii.
Mkuu wa waangalizi wa Jumuiya ya Madola, Rais wa zamani wa Nigeria Olusegun Obasanjo, alisema matatizo mengi katika utaratibu wa uchaguzi yalitia dosari uaminifu na uhaki wa shughuli nzima
Sign up here with your email