WAZIRI MWIJAGE APONGEZA UJENZI WA KIWANDA CHA VIGAE - Rhevan Media

WAZIRI MWIJAGE APONGEZA UJENZI WA KIWANDA CHA VIGAE

EVOWaziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage amepongeza jitihada zinazofanywa na muwekezaji wa kampuni TwyFord Tanzania Cereramics,kwa ujenzi wa kiwanda cha kutengeneza vigae “Tiles” katika Kijiji cha Pingo, Chalinze Mkoani Pwani.
Waziri Mwijage, amesema hayo alipotembelea na kukagua maendeleo ya awali ya eneo, litakalojengwa kiwanda hicho cha kutengeneza vigae “Tiles” kitakachotoa ajira kwa watanzania zaidi ya elfu mbili katika mfumo rasmi,na ajira elfu nne zisizo rasmi.
“kiwanda hiki kikikamilika kitasidia sio tu kutoa ajira lakini pia kitasidia kwa watanzania kununua na kuuza bidhaa zinazotengenezwa nyumani na sio  kuangiza kila kitu kutoa nje”alisema Mwijage.
Waziri Mwijage aliongeza kuwa,” bidhaa hizi pia zitauzwa katika nchi majirani kama Zambia,Malawi, DRC,Rwanda, Burundi,Uganda na Jamhuri ya watu wa Afrika Kati na kusafirishwa nje ya bara.
Aidha Waziri Mwijage alisema kuwa  kiwanda hicho kitumike vizuri na kutoa wito kwa watanzania kutumia fursa zitakazo patikana katika mradi huo zitumike kwa faida ya kila mmoja, “Serikali ya kijiji itambue maeneo yake ili kusaidia kuharakisha maendeleo ya eneo hili ambapo kiwanda kinafanya shughuli zake”alisema Mwijage.
Kwa upande Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete, alisema kuwa ujenzi  wa kiwanda hicho kipo katika hatua ya mwanzo ya Ujenzi na kinataraji kukamilika Mwezi wa Saba na kufunguliwa Rasmi mwezi wa Nane mwaka huu.
 Ridhiwani alisema kuwa kiwanda hicho kitasaidia kufungua mji wa Chalinze na kufanya mji wa viwanda na biashara na hivyo kufungua fursa za kiuchumi na kupanua mji huo,katika sekta ya viawanda inayosimamia vyema na serikali ya awamu ya tano.
 “ujenzi wa kiwanda hiki ni Alama Chanya ya jinsi serikali ya awamu ya Tano ilivyojidhatiti kufungua fursa za viwanda katika Nchi yetu.Wananchi wa Chalinze na Pwani wameaswa kuendelea kujipanga kwa viwanda na fursa nyingi zaidi.”alisema ridhiwani
Ridhiwani aliongeza kwa kunshukuru muwekezaji huyo pia  kwa kukubali kusaidia kumalizia ujenzi wa shule ya sekondari ya kata ya Pera na kituo cha afya katika kata hiyo.
“licha ya kukubali kusaidia  ujenzi wa huo lakini pia fursa nyingine watu watapata  nafasi ya kuuza mali ghafi zinazotumika kutengeza  vigae hivyo ambapo tunatarajia asilimia 90 malighafi hizo zitatoka hapa kwetu katika  mikoa ya jirani”.alisema Ridhiwani.
Previous
Next Post »