WAZIRI MWIJAGE AKAGUA MANDELEO YA AWALI UJENZI WA KIWANDA KIPYA CHA VIGAE, CHALINZE MKOANI PWANI - Rhevan Media

WAZIRI MWIJAGE AKAGUA MANDELEO YA AWALI UJENZI WA KIWANDA KIPYA CHA VIGAE, CHALINZE MKOANI PWANI

Waziri wa Viwanda na Biashara, Charles Mwijage (wa pili kushoto) akiwa ameongozana na Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete (wa tatu kushoto), Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya TwyFord Tanzania Cereramics, Jack Feng (kushoto) wakati walipokuwa wakitembea na kukagua maendeleo ya awali ya eneo litakalojengwa kiwanda kikubwa cha kutengeneza vigae "Tiles" lililopo katika Kijiji cha Pingo, Chalinze Mkoani Pwani. Waziri Mwijage ameridhishwa na maandalizi ya ujenzi wa kiwanda hicho na kumpongeza muwekezaji wake hasa kwa kasi wanayoenda nayo. Kwa mujimu wa Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya TwyFord Tanzania Cereramics ambao ndio wamiliki wa kiwanda hicho, amesema kuwa ifikapo mwanzoni mwa mwezi septemba mwaka huu, kiwanda hicho kitakuwa kimekamilika na kitaanza kufanya kazi. Uwepo wa kiwanda hicho, utaweza kufungua fursa za ajira kwa vijana mbalimbali nchini.
Waziri wa Viwanda na Biashara, Charles Mwijage (katikati) akizungumza jambo Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya TwyFord Tanzania Cereramics, Jack Feng (kulia) wakati alipotembea eneo litakalojengwa kiwanda kikubwa cha kutengeneza vigae "Tiles" lililopo katika Kijiji cha Pingo, Chalinze Mkoani Pwani.
Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwani Kikwete (kulia) akimuonyesha kitu, Waziri wa Viwanda na Biashara, Charles Mwijage wakati walipokuwa wakitembea na kukagua maendeleo ya awali ya eneo litakalojengwa kiwanda kikubwa cha kutengeneza vigae "Tiles" lililopo katika Kijiji cha Pingo, Chalinze Mkoani Pwani.
Waziri wa Viwanda na Biashara, Charles Mwijage akimsikiliza Meneja Uhusiano wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Pendo Gondwe wakati akimueleza jambo, wakati alipotembea eneo litakalojengwa kiwanda kikubwa cha kutengeneza vigae "Tiles" lililopo katika Kijiji cha Pingo, Chalinze Mkoani Pwani.

Previous
Next Post »