MFUKO
wa Sekta Binafsi nchini (TPSF) umesema ujio wa viwanda 200 kutoka
nchini China,Serikali inatakiwa kujipanga kupokea viwanda hivyo kwani
vitachangia kukua kwa uchumi pamoja na ajira nchini.
Akizungumza
na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa
TPSF, Godfrey Simbeye amesema China kwa sasa ni nchi yenye mitaji
mikubwa kuliko nyingine duniani hivyo lazima kuongeza mahusiano zaidi
ili kuweza kunemeeka nao katika kuelekea uchumi wa kati wa viwanda
kufikia 2025.
Simbeye
amesema viwanda vingi vya China vimefikia hatua ya kuweza kuhamishwa
katika sehemu mbalimbali katika Bara la Afrika na kuendelea na
uzalishaji kutokana na uhakika wa rasilimali watu pamoja na malighafi.
Amesema kutokana
na uwekezaji wa viwanda hivyo suala la maeneo tengefu liangaliwe
kimkakati katika kufanya maandalizi ya viwanda hivyo pamoja na
vingine vitakavyojengwa.Simbeye
amesema nchi ya China ina uwezo mkubwa wa mitaji kuliko maeneo mengine
duniani na Tanzania inaelekea katika uchumi wa
viwanda zilizowawezesha kufanya mapinduzi ya viwanda.
Aidha
amesema ujio wa Waziri wa Mambo ya Nchi wa China nchini ni sehemu ya
kuchangamkia fursa kwa karibu kwa kuongeza uhusiano uzidi kudumu ambao
wenye maendeleo baina ya nchi mbili.
.Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Sekta Binafsi Nchini (TPSF), Godfrey Simbeye akizungumza na waandishi habari juu ujio wa viwanda 200 vya China kuhamishiwa Nchini iliyofanyika jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Kitengo cha Masuala ya Uwekezaji na Maendeleo ya Biashara wa TPSF, Edward Furaha akizungumza na waandishi habari juu ujio wa viwanda iliyofanyika jijini Dar es Salaam, Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa TPSF, Godfrey Simbeye.
Sign up here with your email