PUTIN : AFUNGUKA MAZITO KUHUSU MAUAJI YA UBALOZI WA UTURUKI . - Rhevan Media

PUTIN : AFUNGUKA MAZITO KUHUSU MAUAJI YA UBALOZI WA UTURUKI .

Andrei Karlov

Andrei Karlov alikuwa amezuru maonesho ya picha mjini Ankara
Rais wa Urusi Vladimir Putin, amesema kuuawa kwa balozi wa taifa lake nchini Uturuki Andrey Karlov siku ya Jumatatu ni uchokozi ambao lengo lake ni kuvuruga juhudi za kutafuta amani Syria.
Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan, alisema kuuawa kwa balozi huyo ni shambulio dhidi ya taifa la uturuki.
Bw Karlov aliuawa kwa kupigwa risasi na afisa wa polisi ambaye hakuwa kwenye zamu, alipokuwa anatoa hotuba kwenye maonesho ya picha katika mji mkuu Ankara.
Picha za video zilimuonesha mshambuliaji, akiwa amevalia suti na tai, akimfyatulia risasi balozi huyo kutoka nyuma, akisema kwa sauti ujumbe kuhusu mji wa Aleppo, Syria.
Mshambuliaji huyo aliuawa kwa kupigwa risais na polisi.
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeshutumu mauaji hayo.
Taarifa zinasema mwuaji ni Mevlut Mert Aydintas, 22, ambaye alikuwa anahudumu katika kikosi cha polisi kupambana na fujo mjini Ankara.
Haijabainika iwapo ana uhusiano wowote na kundi lolote.
Kisa hicho kilitokea siku moja baada ya maandamano kufanyika Uturuki kupinga hatua ya Urusi kumuunga mkono Rais wa Syria Bashar al-Assad.
Recep Tayyip Erdogan alizungumza na Bw Putin kwa njia ya simu, na kwenye ujumbe wa video, alisema wote wawili walikubaliana kisa hicho kilikuwa "uchokozi".
  Mshambuliaji huyo alizungumza kuhusu Aleppo na Syria
Mshambuliaji huyo alizungumza kuhusu Aleppo na Syria
Alisema wale waliotaka kuharibu uhusiano baina ya nchi hizo mbili hawatafanikiwa.
Bw Putin kwa upande wake alisema "bila shaka ni kisa cha uchokozi chenye lengo la kuvuruga kurejea hali ya kawaida" kwa uhusiano wa kidiplomasia na "shughuli ya kutafuta amani Syria".
Wachunguzi kutoka Urusi wametumwa Uturuki kuchunguza kisa hicho, msemaji wa Bw Putin, Dmitry Peskov amesema.
Katibu Muu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon na Rais wa Ufaransa Francois Hollande amelaani mauaji hayo. Mawaziri wa Marekani, Uingereza, Ujerumani pia wameshutumu mauaji hayo.
Kundi linaloongozwa na kiongozi wa kidini aliyetorokea Marekani Fethullah Gulen pia limeshutumu mauaji hayo na kujitenga na muuaji huyo.
  Watu wakijikinga ukumbini baada ya mshambuliaji kuanza kufyatua risasi
Watu wakijikinga ukumbini baada ya mshambuliaji kuanza kufyatua risasi
Polisi walizingira eneo hilo baada ya tukioPolisi walizingira eneo hilo baada ya tukio
Karlov, 62, ni mwanabalozi wa muda mrefu wa Urusi.
ALihudumu kama balozi wa Muungano wa Usovieti nchini Korea Kaskazini miaka ya 1980.
Baada ya kuvunjika kwa muungano huo mwaka 1991, alihudumu kama balozi Korea Kusini kwa miaka kadha kabla ya kurejea Korea Kaskazini mwaka 2001.
Alitumwa Ankara Julai 2013.
Previous
Next Post »