Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda amewataka wakazi wa Mkoa huo ambao taka zimezagaa eneo la mitaa yao na hazijafuatwa kubebwa wazipeleke nje ya ofisi ya Serikali ya Mtaa na Mwenyekiti atafanya utaratibu wa kuzisafirisha.
" Katika mkoa wangu wa Dar es Salaam sitaki nisikie mazingira yenu machafu kila Mtaa nahitaji uwe msafi. Safisha mazingira yenu mlipie taka ushuru kila mwezi na taka zikitekelezwa bila kuzolewa na Wakandarasi pelekeni ofisi ya Mwenyekiti wenu." alisema Makonda.
Alisema ifike wakati watu wabadilike ili kutunza mazingira yetu kila mmoja kufanya usafi ni wajibu wake.
"Nahitaji mji wa Dar es saalam ubadilike nataka kuona usafi tuepuke mazingira machafu lengo likiwa ni kupambana na mgonjwa ya milipuko,"alisema.
Katika ziara yake Makonda pia alitembelea eneo la Kawe ambapo alitembela nyumba zilizojengwa katika maeneo hatarishi ambapo alitoa agizo kwa TANESCO na DAWASCO kuondoa miundombinu iliyopo katika eneo hilo ili wananchi waondoke katika eneo hilo.
Makonda alisema eneo hilo sio salama kwa makazi ya watu hivyo amewataka wakazi wa eneo hilo kuondoka.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda akisalimiana na Mwenyekiti wa Kikundi cha wa Mama wanaohudumia mzunguko wa Kigogo Elizabeth Matarimo jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda akipokea pipa la kuwekea takataka kutoka kwa Msemaji wa Kiwanda cha Nondo MM Steel,Abuu Mlawa leo jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda akizungumza na wananchi wa Kigogo na kusikiliza kero zao leo jijini Dar es Salaaam.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda, alitembelea eneo la Kawe ambapo alitembela nyumba zilzojengwa katika maeneo hatarishi na kutoa agizo kwa TANESCO na DAWASCO kutoa miundombinu iliyopo katika eneo hilo leo jijini Dar es Salaam.
Sign up here with your email