Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania Mh. Joh Pombe Magufuli, leo amefanya uteuzi wa wenyeviti wa
bodi za hifadhi za jamii hapa nchini, za PSPF na LAPF.
Pia Rais Magufuli amemteua aliyekuwa Makamo Mkuu wa Chuo cha Ushirika Moshi, Prof. Faustine Karani Bee kuwa Mwenyekiti wa Mfuko wa Pensheni wa Serikali za Mitaa (LAPF).
Wakati huo huo Rais Magufuli amemteua Prof. Tadeo Andrew Satta kuwa Mkuu wa Chuo cha Usimamizi wa Fedha IFM, ambaye awali alikuwa akikaimu nafasi hiyo.
Taarifa ya uteuzi huo imetolewa leo na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi, kupitia Kurugenzi ya mawasiliano Ikulu.
Sign up here with your email