KOCHA Hans Pluijm amesema wakati wowote atakabidhi taarifa ya benchi
la ufundi kwa ajili ya kuanza kufanyiwa kazi na Kocha mpya George
Lwandamina anayetarajiwa kuanza kazi mzunguko wa pili wa Ligi Kuu
Tanzania Bara.
Akizungumza , Pluijm alisema taarifa yake
haijakamilika lakini anaendelea kuiandaa na wakati wowote ataikabidhi.
“Nimeanza kuiandaa taarifa, wakati wowote nitakabidhi,”alisema Pluijm huku akisema suala hilo aachiwe yeye na uongozi wa Yanga.
Lwandamina amenukuliwa kwenye vyombo vya habari kuwa anasubiri
taarifa hiyo kuanza kazi mara moja. Lwandamina alisema anaijua Yanga
kupitia DVD alizotazama na huenda akabadilisha kikosi na pengine mfumo.
Hata hivyo, bado uongozi wa Yanga haujatoa taarifa rasmi kuhusu hatma
ya Kocha Hans Pluijm ingawa kunaelezwa kuna mazungumzo ya kumshawishi
Pluijm kuwa Mkurugenzi wa benchi la ufundi, na nafasi ya Kocha iwe ya
Lwandamina.
Kocha huyo Mholanzi alisema ni kweli anaendelea na mazungumzo na Yanga ili kujua hatma yake.
Pluijm hakutaka kuweka wazi juu ya kinachoendelea, ambapo alisisitiza
kuwa uongozi wa Yanga ndio wenye nafasi ya kuzungumzia yale
yanayoendelea kati yao.
Kocha huyo hivi karibuni aliandika barua ya kujiuzulu baada ya Yanga
kufanya mazungumzo ya kumchukua kocha Mzambia bila ya kumhusisha
Mholanzi huyo, ambaye aliahidiwa kupewa ukurugenzi wa ufundi.
Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwigulu Nchemba ndiye aliyemshawishi kufuta uamuzi wake wa awali wa kujiuzulu nafasi hiyo.
Sign up here with your email