MPAKA VIATU RANGI ANAYEVUNA KULIKO WAFANYAKAZI WA UMMA - Rhevan Media

MPAKA VIATU RANGI ANAYEVUNA KULIKO WAFANYAKAZI WA UMMA

 Idris anasema kuwa yeye hupata karibu dola tano kwa siku

Idris, raia wa Nigeria mwenye umri wa miaka 21, amekuwa akipaka viatu rangi kwa muda wa miaka mitatu sasa.
Huwa anazunguka mitaa ya mji wa Abuja akiwatafuta wateja ambao wangependa viatu vyao kushonwa au kupakwa rangi.
Idris hana kisomo lakini hajutii hilo. Anasema kuwa hupata karibu dola 5 kwa siku na kuongeza kuwa kipato chake cha mwezi mzima ni cha juu kuwaliko cha wafanyakazi wengine wa umma, ambao mishahara yao ni kati ya dola 125 na 190.

Ndoto ya Idris ni kumiliki kiwanda kikubwa cha kutengeneza rangi ya viatu, lakini kwa sasa ameamua kuwa mpaka viatu rangi kwenye mitaa ya mji wa Abuja.
Previous
Next Post »