HAKIELIMU YABARIKI MABADILIKO KATIKA MAFUNZO YA UALIMU NCHINI - Rhevan Media

HAKIELIMU YABARIKI MABADILIKO KATIKA MAFUNZO YA UALIMU NCHINI

Kutokana na mabadiliko ya mafunzo ya  ualimu yaliyo fanywa na Wizara ya Elimu ,Sayansi, Tektinolojia na ufundi  novemba mwaka huu  kuondoa  mamlaka ya usimamizi wa ngazi ya cheti  na stashahada  kutoka  Baraza la taifa elimu ya ufundi     NACTE  na kuyarudisha wizara ya Elimu chini ya  uangalizi wa baraza la mitihani Tanzana  NECTA,   shirika lisilo la kiserikali  linalojishughulisha na Elimu nchini (HAKI ELIMU ) limeipongeza Serikali kwa hatua  hiyo kwani hapo awali kwa kushirikiana na wadau wengine wa  Elimu  lilikuwa limesha toa mapendekezo kama hayo lakini hayakufanyiwa kazi.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam  jana, mkurugenzi mtendaji wa HAKI  ELIMU ,Bwana John Kalage alisema  mabadiliko hayo yatasaidia kuinua kiwango cha elimu nchini,ingawa mabadiliko ya awali yalikuwa na lengo jema la kukabiliana na upungufu  mkubwa  wa  waalimu wa kufundisha masomo ya Sayansi katika shule nyingi hapa nchini lakini yalikuwa na athari  ya kuzorotesha ubora wa Elimu.

Alisema ,utaratibu wa kuvifanya vyuo  vya elimu kujitegemea  katika kudahili wanafunzi, kutathimini na kutunza waalimu tarajali ulikuwa pia na athali ya kushusha  kiwango  mafunzo ya ualimu  kwakuwa kila taasisi iikuwa na uhuru wa kujiamulia viwango vya  ubora wa mafunzo  itakayo toa ,

“Katika zama hizi za ushindani kulikuwa na hatari dhahili kuwa  kila taasisi ingeweza kudahili  na kufaulisha wanafunzi wake  hata wasio stahili  ili kuvutia wana chuo wengi zaidi  kwalengo la kujipatia ada ‘’alisema

Hatahivyo  shirika hilo limetoa baadhi ya mapendekezo na kuishauri Serikali  kuunda chombo  chenye mamlaka ya juu katika elimu (Education Reguratory Authority ) chini ya sheria  ya elimu ili  kusimamia na kulinda sera ,sheria ,kanunu na miongozo  ya elimu iliyo wekwa ili  kupunguza  maamuzi na mabadiliko ya mara kwa mara  katika secta ya Elimu

“Kwa sasa ina onekana  waziri ana mamlaka makubwa  makubwa ya kutoa  maamuzi  hali inayo onekana kuwepo kwa nyaraka nyingi  zinazo badilika kia mara hata kabla hazija fanyiwa kazi kikamilifu”

Kalage alisema  nivema  mafunzo ya  ualimu ngazi zote yakaendelea kutolewa na  vyuo vikuu na vyuo vya ualimu peke yake na vyuo vingine visivyo vya ualimu visiruhusiwe kutoa mafunzo hayo kwa kuwa lengo lao sikutoa mafunzo hayo .

"Nibora kuwa na vyuo vichachache ambavyo serikali ina uhakika na uandaaji wake  ili vyuo hivi vilishe shule zote  za umma na bnafsi ,hii itasaidia kuboresha kiwango cha elimu nchini."alisema
Previous
Next Post »