LIL WAYNE ABURUZWA MAHAKAMANI - Rhevan Media

LIL WAYNE ABURUZWA MAHAKAMANI

Lil WayneNEW YORK, Marekani
MWANAMUZIKI wa Hip Hop, Lil Wayne, amejikuta akiingia matatani baada ya kuburuzwa mahakamani na Kampuni ya American Express kwa kosa la kutolipa kodi kwa muda wa miezi sita sasa.
Kampuni hiyo imemfikisha Wayne mahakamani Alhamisi iliyopita ikimtaka alipe pesa anazodaiwa Dola za Marekani 86,396 (Sh mil 185) pamoja na fidia ya ucheleweshwaji wa malipo hayo.
Bado Wayne hajasema lolote kuhusiana na shutuma hizo. Wayne amekuwa na kesi nyingi za aina hii karibu kila mwaka.
Previous
Next Post »