WAPENZI WA JINSIA MOJA WASHAMBULIWA IVORY COAST - Rhevan Media

WAPENZI WA JINSIA MOJA WASHAMBULIWA IVORY COAST


Wapenzi wa jinsia moja nchini Ivory Coast wamekuwa wakidhulumiwa na kulazimishwa kuhama makwao baada ya ubalozi wa Marekani kuchapisha picha yao wakiweka sahihi kwenye kitabu cha rambi rambi kwa waathiriwa wa mauaji yaliyofanyika katika klabu moja ya wapenzi wa jinsia moja mjini Orlando jimbo la Florida nchini Marekani.
Picha iliyochapishwa kwenye mtandao wa ubalozi wa Marekani na kusambazwa kwenye mitandao ya kijamii, ilionyesha wanaume sita wakiweka sahihi kwenye kitabu cha rambi rambi.
Shirika la habari la AP lilizungumza na wanaume hao wote wanne ambao hawakutaka kutajwq majina.
Wawili kati yao wanasema kuwa walisambuliwa na kundi la watu huku wengine wawili nao wakisema kuwa shinikizo za kifamilia zimewalazimu kuhama nyumbani.
Previous
Next Post »