VIONGOZI WA VIJIJI TUMBO JOTO WADAIWA KUTAFANA MAMILIONI YA UJENZI WA MAABARA. - Rhevan Media

VIONGOZI WA VIJIJI TUMBO JOTO WADAIWA KUTAFANA MAMILIONI YA UJENZI WA MAABARA.


VIONGOZI  wa vijiji akiwemo Mtendaji wa kata ya Migato wilaya Itilima Mkoani Simiyu, wametuhumiana kutafuna zaidi ya shilingi Milioni saba zilizokuwa za ujenzi wa maabara mbili zilizomo kwenye kata hiyo.

Viongozi hao walitumia muda wa saa sita kurushiana mpira kwa kila mmoja kuhusika na ubadhilifu wa fedha hizo, hali iliyosababisha kuanza kutaja siku, wakati na mahali walivyotafuna fedha hizo.


Hali hiyo ilijitokeza juzi wakati wa kikao cha maendeleo cha kata (WODC) kilichokuwa chini ya Diwani wa kata hiyo Mbuga Ntobi, pamoja na Kaimu mkurugenzi wa halmashauri Anneth Msofe.

Awali akizungumzia hali ya maabaara hizo katika shule ya sekondari Shishani, pamoja na Mhunze, Diwani huyo alieleza kuwa tangu ameingia madarakani hakuna mwendelezo wa ujenzi wa maabara hizo.

Alieleza kuwa alishangazwa kuona mbao kwa ajili ya kuezeka mabaara zote mbili zikiwa tayari zimeungwa, huku ujenzi wa boma ukiwa katika kozi mbili na kasi yake ikiwa katika kiwango cha chini.

“ Mpaka leo mbao ziko chini zimeungwa na leo ni muda wa mwaka mmoja umepita mbao hizo zimeanza kuoza huku ujenzi ukiwa katika kozi mbili za boma nimekuwa nauliza kwa nini ujenzi umesimama?  sijapata jibu sasa leo lazima tupate jibu hapa hapa” alisema  diwani huyo.

Baada ya diwani kutoa maelezo hayo alimtaka Mtendaji wa kata Logo Sitta kutoa majibu, ambapo alianza kusoma fedha zilizopatikana na matumizi yake wakati wa ujenzi wa maabara hizo.

Taarifa hiyo ilikataliwa na wajumbe wa kikao hicho ambao baadhi yao walikuwa wenyeviti wa vijiji, ambapo walianza kusoma taarifa za kwao ambazo zilikuwa zinakinzana na taarifa ya mtendaji wa kata.

Ndimila Buhula pamoja na Linja Tulutu walieleza kuwa Mtendaji huyo wa kata ndiye chanzo cha ujenzi wa maabara hizo kushindwa kuendelea kutokana na kushindwa kutoa matumizi sahihi ya fedha zilizotoka halmashauri kwa ajili ya ujenzi.


Hatua hiyo ilimfanya Mtendaji wa kata kuanza kueleza jinsi fedha hizo zilivyotumika, ambapo alibainisha kuwa baadhi ya fedha walitumia kwa ajili ya kupeana posho usafiri pamoja na chakula kwenye vikao vya wajumbe wa kamati ya ujenzi wa maabara .

.

Hali hiyo ilizua mzozo mkubwa kutoka kwa wenyeviti hao ambao walikana na kudai kuwa vikao vyote kwenye kamati hawajawahi kula chakula wala kupewa posho, huku wakieleza walimsikia mtendaji akiomba ten Parcent (rushwa) kutoka kwa mkandarasi alipewa kazi ya ujenzi.

Mbali na hilo walieleza kuwa mtendaji huyo alisaidia Mkandarsi huyo kukimbia na fedha za ujenzi ambazo alilipwa na mtendaji bila ya kuwepo wajumbe, na mpaka leo mkandarasi wahajui mahali alipo.

Baada ya hali hiyo ilibainika kuwa jumla ya shilingi Milioni 7,430,250 zilitafunwa na viongozi hao wakiongozwa na mtendaji wa kata, ambapo kikao kiliazimia warejeshe fedha hizo mara moja.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi huyo ambaye pia  ofisa utumishi, alimtaka  mtendaji wa kata  kuhakikisha fedha  hizo  zinarejeshwa haraka  na  hatua za kisheria zitachuliwa dhidi yake.
Previous
Next Post »