Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa akihakiki usahihi wa moja ya kifaa cha kupimia hali ya hewa katika ofisi za Mamlaka hiyo mkoani Singida. Kushoto ni Meneja wa Mamlaka ya Hali ya Hewa mkoani Singida Bw. Florian Rweyongeza. Mkurugenzi wa Kampuni ya Simu nchini (TTCL), Kanda ya Kaskazini Bw. Peter Lusama(wa tatu kulia), akitoa taarifa kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa (wa pili kulia), kuhusu maendeleo ya ujenzi wa mkongo wa taifa mkoani Singida. Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa akitoa maelekezo kwa Mkurugenzi wa Kampuni ya Simu nchini (TTCL), Kanda ya Kaskazini Bw. Peter Lusama umuhimu wa kupitisha mkongo wa mawasiliano juu katika eneo la Msamvu linaloathiriwa na mafuriko mara kwa mara mkoani Singida. Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa akijadiliana jambo na Mkurugenzi wa TEHAMA kutoka sekta ya Mawasiliano Eng. Peter Mwasalyanda wakati akikagua kituo cha kutunza taarifa mbalimbali (data centre), jijini Dar es Salaam. Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa akitizama kwa karibu mtambo wa kuratibu usalama katika kituo cha kutunza taarifa mbalimbali (data centre) jijini Dar es Salaam. Kituo hicho cha kwanza kujengwa nchini kitatunza taarifa za Serikali na sekta binafsi.