Bendera kote nchini Uturuki zilipeperuka nusu mlingoti Jumatano pale taifa hilo lilipoadhimisha siku ya maombolezi kufwatia shambulizi la wajitoa mhanga 3 Jumanne katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Ataturk mjini Istanbul. Wanusura wamekuwa wakieleza yale waloshuhudia na kutuma ujumbe wa ujasiri, Kama msafiri kutoka Hungary, Dorka Kardosh.
Kardosh alisema, anadhani hatupaswi kuwa waoga kwa sababu hilo ndilo lengo lao, lakini hatuwezi kuishi maisha yetu tukiogopa kwenda nje.
Wafatiliaji wanasema mamlaka za Uturuki zimehakikisha kutuma ujumbe kuwa Istanbul bado ni jasiri. Masaa tu baada ya mashambulizi, uwanja wa ndege wa Ataturk ulifunguliwa tena. Vikosi vya usalama vya Uturuki viko katika harakati za kuwatambulisha wajitowa mhanga hao. Washambuliaji wanaonekana kuwa walijiandaa na kujiratibu vyema. Kabla ya kujiripua, washambuliaji walokuwa wamejihami vyema, walishambulia watu kwa bunduki na bastola katika eneo la kuwasili abiria wakimataifa, ambalo lilikuwa limejaa watu.
Uwanja wa ndege wa Ataturk ni mojawapo ya viwanja vya ndege vilivyo na shughuli nyingi duniani. Waziri mkuu wa Uturuki Binali Yidirim, akizungumza baada ya shambulizi, alililaumu kundi la Islamic state.
Kwa mujib wa taarifa za awali kutoka kwa maafisa wa uslama wa Uturuki, shambulizi linaonekana kuwa limefanywa na kundi la Daesh, ambalo ni jina jengine la kundi la Islamic State. Mkuu wa shirika la kijasusi la Marekani John Brennan alisema Jumatano kuwa shambulizi hilo linaonyesha ishara za kile alichokiita uasi wa Islamic State.
Bw Yildirim alitowa wito wa umoja wa kitaifa, lakini wafatiliaji wanaonya kuwa shambulizi huwenda likazidisha migawano ya kisiasa. Vyama vya upinzani vinaishutumu serikali kwa kushindwa kupambana zaidi na kundi la Islamic state ambalo linaaminiwa kuwa na mtandao mkubwa nchini humo.
Vituo vya habari vinaripoti kuwa idara ya kijasusi ya Uturuki ilitowa onyo wiki kadhaa zilizopita kuwa Istanbul inakabiliwa na kitisho cha shambulzi kutoka kwa Islamic State. Wachambuzi wanasema kundi hilo la wanajihadi ambalo limekosa ushindi wa kijeshi huko Iraq na Syria ,litakuwa na ari ya kufanya shambulizi la kulipiza kisasi. .
KIKOSI CHA TWIGA STARS KIPYA CHATANGAZWA-MAJINA HAYA HAPA
Kocha
Mkuu wa timu ya taifa ya Mpira wa Miguu ya Wanawake Tanzania, Nasra
Juma ametangaza majina ya wachezaji 23 watakaounda kikosi cha Twiga
Stars.
Kikosi
hicho kinatarajiwa kwenda Kigali, Rwanda Julai 15, 2016 kucheza mchezo
wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya timu ya taifa ya Rwanda ikiwa ni
mwaliko maalumu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu la Rwanda (Ferwafa).
Wakati
Ferwafa likiingiza mchezo huo wa Julai 17, 2016 kwenye orodha ya
michezo inayotambuliwa na Shirikisho la Mpira na Miguu la Kimataifa
(Fifa), lakini Mheshimiwa Rais wa Rwanda Paul Kagame kuwa sehemu ya
burudani ya burudani mbele ya wageni wake ambao ni wakuu mbalimbali
wanaounda Umoja wa Nchi za Afrika (AU) ambao watakuwa na mkutano wao
nchini Rwanda.
Mbali
ya soka kama burudani, pia Rais Kagame atatumia mchezo huo kama hamasa
kwa wakuu wa nchi ili kutoa kipaumbele kwenye soka la wanawake ambako
kwa sasa ni ajira ambayo inakwenda sambamba na kuitikia wito wa
kupambana na changamoto za malengo ya millennia (MCC) ambayo pia
yanataka wanawake wapate nafasi.
Makipa:
- Fatma Omary
- Belina Julius
- Najiat Abbas
Walinzi:
- Stumai Abdallah
- Fatma Issa
- Anastazia Antony
- Happuness Henziron
- Maimuna Khamis
Viungo:
- Donisia Daniel
- Amina Ali
- Amina Ramadhani
- Fatuma Bashiri
- Wema Richard
- Fadhila Hamadi
- Mwajuma Abdallah
- Anna Hebron
- Sophia Mwasikili
Washambuaji:
- Tumaini Michael
- Johari Shaaban
- Fatma Idd
- Shelder Bonifdace Mafuru
- Asha Saada Rashid
- Mwanakhamisi Omar
…………………………………………………………………….
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA SOKA TANZANIA
KIKOSI CHA TWIGA STARS KIPYA CHATANGAZWA-MAJINA HAYA HAPA
Kocha
Mkuu wa timu ya taifa ya Mpira wa Miguu ya Wanawake Tanzania, Nasra
Juma ametangaza majina ya wachezaji 23 watakaounda kikosi cha Twiga
Stars.
Kikosi
hicho kinatarajiwa kwenda Kigali, Rwanda Julai 15, 2016 kucheza mchezo
wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya timu ya taifa ya Rwanda ikiwa ni
mwaliko maalumu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu la Rwanda (Ferwafa).
Wakati
Ferwafa likiingiza mchezo huo wa Julai 17, 2016 kwenye orodha ya
michezo inayotambuliwa na Shirikisho la Mpira na Miguu la Kimataifa
(Fifa), lakini Mheshimiwa Rais wa Rwanda Paul Kagame kuwa sehemu ya
burudani ya burudani mbele ya wageni wake ambao ni wakuu mbalimbali
wanaounda Umoja wa Nchi za Afrika (AU) ambao watakuwa na mkutano wao
nchini Rwanda.
Mbali
ya soka kama burudani, pia Rais Kagame atatumia mchezo huo kama hamasa
kwa wakuu wa nchi ili kutoa kipaumbele kwenye soka la wanawake ambako
kwa sasa ni ajira ambayo inakwenda sambamba na kuitikia wito wa
kupambana na changamoto za malengo ya millennia (MCC) ambayo pia
yanataka wanawake wapate nafasi.
Makipa:
- Fatma Omary
- Belina Julius
- Najiat Abbas
Walinzi:
- Stumai Abdallah
- Fatma Issa
- Anastazia Antony
- Happuness Henziron
- Maimuna Khamis
Viungo:
- Donisia Daniel
- Amina Ali
- Amina Ramadhani
- Fatuma Bashiri
- Wema Richard
- Fadhila Hamadi
- Mwajuma Abdallah
- Anna Hebron
- Sophia Mwasikili
Washambuaji:
- Tumaini Michael
- Johari Shaaban
- Fatma Idd
- Shelder Bonifdace Mafuru
- Asha Saada Rashid
- Mwanakhamisi Omar
…………………………………………………………………….
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA SOKA TANZANIA
Sign up here with your email
