WATU 46 WEMRIPOTIWA KUUAWA KATIKA GHASIA ZINAZOENDELEA NCHINI BURUNDI. - Rhevan Media

WATU 46 WEMRIPOTIWA KUUAWA KATIKA GHASIA ZINAZOENDELEA NCHINI BURUNDI.


Watu 46 wameripotiwa kuuawa ndani ya kipindi cha miezi mitatu ya mwanzoni mwa mwaka huu katika ghasia zinazoendelea nchini Burundi.

Wizara ya Usalama wa Uma nchini Burundi imetangaza kuendelea machafuko ambapo watu 46 wameuawa tokea mwanzoni mwa mwaka huu wa 2016 pekee. Kwa mujibu wa wizara hiyo katika machafuko hayo, watu wengine 215 wamejeruhiwa.

Hata hivyo Alain-Guillaume Bunyoni Waziri wa Usalama wa Uma nchini humo ameongeza kuwa, hali ya mambo imeboreka kidogo mwezi huu wa April ikilinganiswa na miezi iliyopita. 

Amewatuhumu wapinzani wa serikali kuwa waroho wa madaraka na kuwahusisha na machafuko hayo yenye lengo la kuharibu usalama wa taifa hilo. Mwaka mmoja umetimia tangu Burundi itumbukie katika hali ya mchafukoge mwezi Aprili mwaka jana, kufuatia hatua ya chama tawala cha CNDD-FDD kumuidhinisha Rais Pierre Nkurunziza kugombea tena urais katika uchaguzi uliopita nchini humo.
Previous
Next Post »