Mtendaji Mkuu wa Shirika la Maji safi na Usafi wa Mazingira jijini Dar es Salaam (DAWASCO) Mhandisi Cyprian Luhemeja akifurahia jambo na ujumbe kutoka Mtandao Kijinsia Tanzania (TGNP) walipofika ofsini hapo kwa ajili ya kutoa shukrani zao.
Mwanaharakati kutoka mtandao wa kijinsia Tanzania (TGNP),
Bi Gema Akilimali akizungumza na waandishi wa habari wakati akitoa shukrani
fupi kwa uongozi wa DAWASCO kutokana na jitihada zilizofanyika katika kuboresha
huduma ya Majisafi na Majitaka Jijini Dar es salaam hususani maeneo ya wananchi
wenye kipato cha chini. Kushoto kwake ni Afisa Mtendaji Mkuu wa Dawasco
Mhandisi Cyprian Luhemeja.