Mkutano Mkuu wa kijiji cha Mgwasi kata ya Makanya wilaya ya Same wa kujadili kero za wananchi umevurugila baada ya mwenyekiti wa kijiji kukataa kujadili ajenda ya kuuzwa kwa eneo la hekta nane linalo chimbwa madini ya Road Light ambalo viongozi wa kijiji wanadaiwa kuliuza kwa mwekezaji kwa kiasi cha shilingi laki sita na wananchi wametoa wiki mbili za mwekezaji huo kuondoka kwenye eneo ilo la sivyo watafanya maamuzi magumu.
Katika mkutano huo uliohudhuliwa na idadi kubwa ya wakazi wa kijiji cha Mgwasi uligubikwa na sintofahamu baada ya mwenyekiti wa kijiji hicho Abraham Arevo kuwakilisha hoja moja tu ya Madawati badala ya kujadili kero ya kuuzwa kwa ardhi kisha wananchi wakaikataa hoja hiyo kuwa siyo kero yao na wakataka kupata maelezo ya ardhi hiyo ya kijiji inayodaiwa kuuzwa kinyemera.
Wakizungumza baada ya kuvunjika kwa mkutano huo wananchi walioonekana kuwa na jazba wamesema awakubaliani na hatua ya viongozi wa kijiji kuuza ardhi ya wananchi tena eneo lenye madini kwa mkataba wa kujengewa Choo cha shule kwa ghalama la shilingi laki sita.
Afisa Mtendaji wa kata ya Makanya Ramadhani Bakari amesema alivyo hamia kwenye Kata hiyo alikuta mkataba umeshasainiwa na alimwita mwekezaji na mwekezaji alionesha nyaraka halali ikiwemo leseni ya uchimbaji hata hivyo ITV inafanya juhudi za kumtafuta mwekezaji wa kampuni ya Hamex General Trading Company ili kupata ukweli wa jambo ilo baada ya kutokuwepo kwenye mkutano huo wa kijiji.
Sign up here with your email