SIMBA YACHINJWA KOMBE LA SHIRIKISHO. - Rhevan Media

SIMBA YACHINJWA KOMBE LA SHIRIKISHO.

Image captionKikosi cha Simba kimeondolewa Kombe la Shirikisho
Hatua ya Robo fainali ya mwisho ya michuano ya Kombe la Shirikisho Tanzania (Federation Cup) imepigwa kati ya Coastal Union dhidi ya Simba katika Uwanja wa Taifa Jijini Dar es Salaam na huku coastal Union
ikifanikiwa kuitoa Simba katika michuano hiyo kwa ushindi wa Bao 2-1.
Magoli ya coastal yamefungwa na Mchezaji wa Cameroon Youssouf Sabo,huku goli la Simba likifungwa na Mganda Hamisi Kiiza.
Coastal sasa inajumuika na Yanga, Azam FC na Mwadui kwenye Droo ya kupanga Mechi za hatua ya Nusu Fainali itakayofanyika Jumanne .
Mshindi wa Michuano hili ataiwakilisha Tanzania mwaka 2017 katika Mashindano ya Kombe la Shirikisho Afrika (CAF).
Previous
Next Post »