Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Joseph Mkirikiti, amewasimamisha kazi watumishi wawili wa halamshauri ya wilaya ya Ukwerewe, kwa tuhuma za ushiriki wa uwepo wa wafanyakazi hewa katika halmashauri hiyo.
Mkuu wa Wilaya ya Ukerewe Joseph Mkirikiti,
Akizungumza na wakuu wa idara na watumishi wa halmashauri hiyo mjini Nansio Wilayani Ukerewe Mkirikiti amewataka watumishi hao kubadilika na kuacha kufanya kazi kwa mazoea jambo ambalo linarudisha nyuma maendeleo.
Mkirikiti amesema kuwa watumish iwanatakiwa kufanya kazi ambazo zitakua na tija kwa wananchi kwa kuondokana na mzigo wa matatizo yanayowakabili lakini sio kuhudhuria ofisini lakini unachofanya kwa wananchi hakionekani.
Akizungumzia suala la Watumishi waliohusika na uwepo wa wafanyakazi hewa ambao wameisababisha hasara serikali ameagiza katibu wa utumishi wa halmashauri na mtumishi wa idara ya utawala wa rasimali watu kusimamishwa kazi na vyombo vya dola vichukue hatua dhidi yao.
Sign up here with your email
