Na Woinde Shizza, Karatu
Wananchi wa kijiji cha Losteti kilichopo katika kata ya mbulumbulu
wilayani karatu mkoani Arusha wamelalamika mamlaka ya hifadhi ya
ngorongoro kwa kitendo cha kuwanyanganya eneo lao la kuchungia mifugo
lijulikanalo kwa jina la Olorieni lililopo ndani ya kijiji hicho.
Wananchi hao waliyasema hayo juzi wakati wakiongea na waandishi wa
habari kijijini hapo na kusema kuwa mamlaka hiyo ya hifadhi ya
ngorongoro wamewanyanganya eneo hilo ambalo walikuwa wanatumia kama
eneo la malisho ya mifugo yao kwa kipindi cha muda mrefu kwani
walianza kulitumia tangu enzi za mababu zao .
Mmoja wa wananchi hao aliyejitambulisha kwa jina la Aron Saiteu
Alisema kuwa eneo hilo la malisho ya mifugo ni lakwao kwa mdua mrefu
lakini wanashangaa kuona hifadhi hiyo ya ngorongoro imekuja na
kuwanyanganya hali ambayo inawafanya hata wao kukosa sehemu ya kufugia
mifugo yao.
Walisema kuwa walishapeleka malalamiko mara kwa mara katika ofisi za
viongozi wa serekali pamoja na ofisi za hifadhi hiyo lakini amna hatua
yeyote ambayo imechukuliwa wala kupewa majibu ambayo yanawapa
matumaini hali ambayo imepeleka wananchi hao kuumia na kukata tamaa
ndani ya nchi yao.
Sign up here with your email