DUDU JINGINE BANDARI YA DAR. - Rhevan Media

DUDU JINGINE BANDARI YA DAR.

Ticts ni kampuni ya kimataifa ya huduma za makontena inayosimamia na kuhifadhi makontena katika bandari ya Dar es Salaam.Pia ni mwanachama wa kampuni ya kimataifa ya CK Hutchison Holdings inayofanya kazi katika bandari 52 kwenye nchi 26 duniani. 

Baada ya kuibuka sakata la mita za kupimia mafuta na ukwepaji wa kodi kwa makontena bandarini, Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) imebainisha kashfa nyingine kwenye kitengo cha mizigo kinachoendeshwa na Kampuni ya Kimataifa ya Huduma za Makontena (Ticts).
Ripoti hiyo iliyotolewa mapema wiki hii imebaini Ticts imevunja taratibu za mkataba na hivyo kusababisha kuikosesha mapato Mamlaka ya Bandari ya Tanzania (TPA).
CAG Mussa Juma Assad ameonyesha katika ripoti ya ukaguzi wa mashirika ya umma kuwa Ticts ilianza kuvunja makubaliano ya mkataba na TPA baada ya kubadilisha umiliki wa asilimia 51 wa hisa za Ictis zilizoko kampuni ya Ticts kwenda Hutchison International Port Limited (HPH).
TPA iliingia makubaliano kwa upande mmoja na Ticts na kampuni ya Huduma za Makontena ya Kimataifa (Ictis) Mei, 2000 ili kuendesha na kusimamia kitengo cha makontena na ghala lililopo Kurasini jijini Dar es Salaam kwa miaka 10.
Katika mkataba huo ulioanza utekelezaji Septemba 2000, Ticts ilitakiwa kuilipa TPA dola 3.68 milioni za Marekani (Sh7.9 bilioni) zilizotakiwa kulipwa siku ya kwanza ya mkataba kwa miezi 12 iliyofuata.

Previous
Next Post »