Makamu
wa rais mteule wa Marekani Mike Pence, amethibitisha kuwa Mitt Rombey
anaweza kupewa wadhifa wa Waziri wa mashauri ya nchi za kigeni.
Taarifa
hiyo iliyotangazwa na kituo cha Fox News, inajiri baada ya rais Mteule
Donald Trump kukutana na bwana Romney, mwanachama wa Republican ambaye
alimkosoa wakati wa kampeni.Kuna uvumi kuwa wadhifa huo ulizungumziwa wakati wa mkutano kati ya viongozi hao.
Hakuna hata mmoja kati yao alitoa taarifa za mkutano wao uliofanyika siku ya Jumamosi.
Mwezi machi wati wa mchujo, bwana Romney alisema kuwa Trump hana tajriba ya kuwa rais naye Trump akajibu kuwa Romney ni mgombea aliyeshindwa.
Sign up here with your email