Idadi ya watu waliyofariki kutokana na ajali ya treni
iliyotokea mapema leo kaskazini mwa India, imeongezeka hadi tisini na
tisa na kuwajeruhi mamia ya wengine. Treni hiyo ilikuwa ikitoka
Indore kuelekea Patna kabla ya kupoteza muelekeo na kutoka katika
barabara ya reli na kuanguka ilipokaribia mji wa Mashariki wa Kanpur
katika jimbo la Utter Pradesh.
Image copyrightAFPImage caption
Wengi wa waliokufa walikuwa kwenye mabehewa yaliyokuwa karibu na injini
Maafisa wa kutoa huduma za dharura wanajaribu kuwaokoa manusura waliokwama katika mabehewa yaliyoanguka. Waziri wa uchukuzi wa India ameamuru kufanywa kwa uchunguzi kubaini kilichosababisha ajali hiyo.